• Login
    View Item 
    •   MKSU Digital Repository Home
    • Conferences / Workshops / Seminars
    • Conferences
    • 1st International Conference
    • View Item
    •   MKSU Digital Repository Home
    • Conferences / Workshops / Seminars
    • Conferences
    • 1st International Conference
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    Kiswahili na Maendeleo Mashambani Nchini Kenya

    Thumbnail
    View/Open
    Full Text (183.0Kb)
    Date
    2018-04
    Author
    Saidi, Makoti V.
    Metadata
    Show full item record
    Abstract
    Makala hii itatathmini umuhimu wa lugha (Kiswahili) katika kuchangia maendeleo nchini Kenya. Maendeleo yamejelezwa na wataalamu mbalimbali. Chambers (1997) ameeleza ‘maendeleo’ kwa usahili kabisa kuwa ni ‘mabadiliko mazuri’ (nchini au duniani). Alan Thomas (2000) ameyaeleza kama kuboreka kwa hali ya maisha, afya na maisha bora kwa wote na mafanikio ambayo huleta uzuri wa maisha kwa jamii yote. Haya hutokea kwa awamu ya muda mrefu. Maendeleo kwa jumla humaanisha mabadiliko chanya ya mwanadamu katika harakati zake zote za kimaisha.Maendeleo ni lazima kwa mwanadamu duniani. Hakuna wanadamu wanaobaki kama walivyo miaka nenda miaka rudi. Kuna maendeleo ya kibinafsi na ya kijamii. Yote haya huwezeshwa na kiwango cha uchumi. Uchumi hukua kutokana na uzalishaji mali. Uzalishaji mali hutokea katika mashamba na mitambo au viwanda. Uwezo huu huletwa na jamii kujifunza mbinu na stadi za uzalishaji mali. Mtu anapojifunza stadi fulani, lazima atumie lugha, lugha anayoielewa. Kwa hivyo, stadi haziletwi na Kiingereza bali lugha yoyote ile. Nchi nyingi ulimwenguni hazitumii Kiingereza na zimeendelea sana, mfano Ujarumani, Ufaransa, Italy, Malasyia, Korea Kisini na kadhalika. Kwa hivyo, natujiulize, je, hapa Kenya tunaweza kutumia Kiswahili kujifunza mbinu na stadi mbali mbali za kuzalisha mali? Hii ni kwa sababu Kiswahili ni somo la lazima nchini kutoka shule za msingi hadi shule za sekondari. Aidha ni lugha rasmi na ya taifa. Hivyo ni lingua franca nchini. Katika makala hii ninajaribu kudadisi swala hili na kutoa mifano kadhaa iliyopatikana nchini Kenya. Maneno makuu: maendeleo, uchumi, mawasiliano, lugha, elimu
    URI
    http://ir.mksu.ac.ke/handle/123456780/719
    Collections
    • 1st International Conference [82]

    DSpace software copyright © 2002-2015  DuraSpace
    Contact Us | Send Feedback
    Theme by 
    @mire NV
     

     

    Browse

    All of Digital RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsBy Submit DateThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsBy Submit Date

    My Account

    LoginRegister

    DSpace software copyright © 2002-2015  DuraSpace
    Contact Us | Send Feedback
    Theme by 
    @mire NV